0


Mgombea ubunge kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi Mh. Davis Mosha Leo jioni amefanya ziara ya Ghafla katika Hospitali ya Mawenzi mjini Moshi kujionea mazingira halisi ya hospitali hiyo hasa zaidi katika wodi ya Wazazi. 


Mh. Davis Mosha akiingia Hospital ya Mawenzi.

Mh. Davis Mosha alichukua maamuzi hayo kwa kusitisha ratiba yake ya jioni na kwenda katika hospitali hiyo baada ya kukutana na Mama mmoja mkazi w kata ya Pasua na kulalamika gharama kubwa wanayotozwa wakina mama katika kupata huduma ya kujifungua. Alikizungumza kwa uchungu mama huyo ambaye mtoto wake amelazwa katika wodi hiyo amejikuta akulipa zaidi ya shilingi laki moja huku akitozwa kiasi cha shilingi elfu Tano kama tozo ya kitanda baada ya siku tatu za bure za kukaa hospialini hapo. 


Mh. Davis Mosha akizungumza na Mzazi ndani ya Wodi ya wazazi.

Davis Mosha alishangazwa na malalamiko hayo huku akifahamu huduma kwa wajawazito hutolewa bure katika hospitali hiyo kwa mujibu wa taarifa ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ambayo inaongozwa na Chadema. Mh Davis alienda na kujiopnea hali halisi na kuzungumza na wamama wajawazito na ambao walikua wamekwisha jifungua na kukuta malalamiko hayo ni kweli na kugundua kuwa wananchi wa Moshi wanadanganywa kwa taarifa ambazo si kweli na wanapopata matatizo hujikuta wakikabiliana na gharama ambazo zinawalazimu kuzilipa ili kupata huduma.

Mh. Davis Mosha akiwa na mmoja wa watoto mapacha waliozaliwa leo.

Mh. Davis Mosha aliwaasa wakina mama hao kuweza kutumia kura yao kwa usahihi katika kipindi hichi cha uchaguzi ili kumchagua kiongozi ambaye hatodanganya na atawatekelezea ahadi zao ipasavyo. Pia aliwea kuweka wazi kuwa huduma nzuri kwa wajawazito ipo katika ilani ya Chama cha mapinduzi na ndio ilani pekee inayotekelezeka cha muhimu ni kuchagua CCM ili kuweza kutekeleza mahitaji hayo.


Mh. Davis Mosha akizungumza na wazazi dani ya Wodi ya Wazazi Mawenzi.
Ikumbukwe Mh. Davis Elisa Mosha ni Mgombea Pekee ambaye anaweza kuleta mabadiliko ndani ya jimbo la Moshi na itakapofika mwezi oktoba 25 usisite kutoa kura yako ya ndio kwake.

Mh. Davis Mosha akiwa na Mtoto ndani ya Wodi ya Wazazi Mawenzi.



Post a Comment

 
Top