0

Mgombea Ubunge kupitia Tiketi ya Chama cha mapinduzi ndani ya jimbo la Moshi Mjini Mh. Davis Elisa Mosha  Amepokea barua ya kutambuliwa rasmi kama mgombea ubunge kupitia ccm, Barua hiyo aliyopokea mapema leo katika ofisi chama cha mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Ndugu Davis Mosha alishukuru sana wanachama wa chama cha mapinduzi kwa kumuamini na kumpa ridhaa ya kuwakilisha katika nafasi hiyo yenye dhamana kubwa katika uongozi.
Baada ya kupokea barua hiyo Mh. Davis Mosha alikutana na waandishi wa habari katika Hoteli ya Nyumbani Hotel na kuzungumza nao juu ya Adhma yake ya kulikomboa Jimbo la Moshi Mjini. Aliweza kuzungumzia mustakabali wa jimbo la Moshi huku akitoa wito kwa wakazi wa Moshi mjini kujitokeza katika mikutano yake na kusikiliza sera na mikakati yake ya maendeleo ndani ya jimbo la Moshi ili kuweza kumpima na kufanya maamuzi sahihi.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari Mgombea ubunge huyo aliweka wazi juu ya tetesi zilizokua zimezagaa kuhusu jina lake kukatwa na kamati kuu ya ccm. Davis alisema Chama cha mapinduzi kina imani nae na kimetumia demokrasia na kuthamini maamuzi ya wanachama wake wa jimbo la Moshi lakini pia wanaamini Jimbo la Moshi linahitaji mtu sahihi mwenye weledi wa uongozi na mwenye uwezo wa kuleta maendeleo Jimboni



Mh. Davis mosha akizungumza na makatibu wa ccm wa kata ndani ya ukumbi wa ccm mkoa mapema leo baada ya kutambulishwa rasmi kama mgombea ubunge ndani ya jimbo la Moshi mjini.



Mamia ya Makatibu wa ccm wilaya ya Moshi mjini wakimsikiliza Mh. Davis Mosha a.k.a Jembe ndani ya ccm Mkoa leo.
  Mh. Davis mosha akionesha barua Rasmi ya kuchaguliwa kugombea ubunge ndani ya Jimbo la Moshi Mjini mbele ya waandishi wa habari.


Mwandishi wa Habari akiuliza swali kwa Mh Davis Mosha

Mh. Davis mosha akifafanua jambo kwa waandishi wa habari

Wandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mh Davis Mosha



Post a Comment

 
Top